Simba SC

MOHAMED HUSSEIN ACHEKELEA KUTWAA TAJI LA LIGI KUU BARA

admin July 19, 2021 4:47 pm


MOHAMED Hussein, nahodha wa Simba amesema kuwa ni furaha kwao kuweza kutwaa taji la Ligi Kuu Bara kwa mara ya nne mfululizo. 

Juzi, Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes ilikabidhiwa taji hilo baada ya ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Namungo FC.

Kwa msimamo ipo na jumla ya pointi 83 baada ya kucheza jumla ya mechi 34 msimu wa 2020/21.

Hussein amesema:”Kila kitu kipo sawa na ni furaha kwetu kuona kwamba tunatwaa ubingwa wa ligi na kila mmoja anafurahi kuona tumeshinda.

“Mashabiki wetu wanahitaji shukrani kwa kuwa wamekuwa nasi bega kwa bega hivyo ni furaha kuona tumefanikiwa kufanya hivyo,” .

MUDATHIR AWEKA REKODI YAKE AZAM FC MAKAMBO AAGWA RASMI HOROYA, DILI LAKE KUTUA YANGA LAWA JEPESI

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply