KIUNGO wa Simba, Hassan Dilunga amesema kuwa walikuwa bora kipindi cha kwanza jambo ambalo limewafanya waweze kupata ushindi wa mabao 2-0 mbele ya KMC , jana Uwanja wa Mkapa.
Kuhusu kuingia akitoka benchi na kubadili mchezo amesema kuwa ni suala la kusoma mchezo. Pia amegusia kuhusu kupoteza kwao mbele ya Yanga wa kufungwa bao 1-0 kwamba hakujawafurahisha hivyo suala hilo wanamuachia Mungu.