kimataifa

MANCHESTER UNITED BADO WANAAMINI WATAMPATA HAALAND

admin August 7, 2021 7:46 am


 MANCHESTER United inaamini kwamba itafanikiwa kuipiga bao Chelsea kwa kumpata staa wa Borussia Dortmund, Erling Haaland.

Haaland kwa sasa amekuwa akitajwa kuwa huenda akajiunga na United ama Chelsea ambazo zimekuwa zikiwania saini yake.

United walikuwa wanahitaji kumpata nyota huyo tangu alipokuwa RB Salzburg lakini ikashindikana, Januari 2020 akatua ndani ya Dortmund alipo kwa sasa.

Kocha wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer anaamini kwamba atampata mshambuliaji huyo na amekuwa akiwasiliana naye mara kwa mara.

Chelsea wao wapo tayari kuweka dau la pauni milioni 150 kupata saini ya nyota huyo huku United wao wakiamini kwamba kama watamkosa msimu huu basi watakomaa kuipata saini yake msimu ujao. 

U 23 MNASTAHILI PONGEZI, KAZI INAENDELEA KWA WAKUBWA VIDEO: LIVE MKUTANO MKUU WA TFF

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply