News

HII HAPA TIMU MPYA MATAJIRI WA LIGI DARAJA LA KWANZA INAYOTAKA KUMSAJILI HAMIS TAMBWE

admin August 18, 2021 8:49 am


DTB FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, imethibitisha nia yao ya kumrudisha nchini straika maarufu Mrundi, Amissi Tambwe.

Tambwe aliyewahi kucheza katika klabu za Simba na Yanga anasifika kwa utupiaji nyavuni na Katibu Mkuu wa DTB, Muhibu Kanu amesema; “Ni kweli tuko kwenye mazungumzo, tukikubaliana atakuja.”

Habari za uhakika kutoka kwa mtu wa karibu na mchezaji huyo alilidokeza  kwamba Tambwe anarejea nchini wakati wowote kuanzia jana baada ya kumalizana kila kitu na mmoja wa vigogo wa timu hiyo.

“Tambwe anarejea nchini kuanzia wiki hii, ameshaelewana kila kitu na bosi wa timu hiyo na anakuja kusaini mkataba, ameamua kuja huku kwa sababu ameona timu hiyo inajipanga kupanda Ligi Kuu,” kilisema chanzo hicho.

Wakati huo huo, inaelezwa vigogo wa klabu hiyo wapo kwenye mipango ya kumrejesha nchini Tafadzwa Kutinyu, raia wa Zimbabwe aliyewahi kucheza Singida United na Azam FC.

YANGA KAMILI GADO KWA MSIMU UJAO, KAZI INAENDELEA SIMBA: KAMBI YA MOROCCO IPO VIZURI,JEZI MPYA KUTAMBULISHA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply