Simba SC

BAADA YA KUPIGWA BEI… KWA MARA YA KWANZA MIQUISSONE AFUNGUKA HAYA KUHUSU SIMBA

admin August 19, 2021 1:55 pm


Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Msumbiji, Luis Miquissone ameaga rasmi Simba SC.

Miquissone amefanya jambo hilo la kiungwana kwa kuweka ujumbe kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii, akiwalenga wachezaji, mashabiki, wanachama na viongozi wa Simba SC.

“Ndugu Familia ya Simba, Asante kwa kunipenda kama mmoja wenu, Asante kwa Bodi, Mwenyekiti, Mkurugenzi Mtendaji, Uongozi wote, Wafanyakazi na wachezaji wenzangu”.

“Siwezi kusahau mashabiki wetu, mtakuwa siku zote moyoni mwangu. Haikuwa uamuzi rahisi kuondoka Simba, lakini ninahitaji kuchukua hii changamoto inayofuata.” ameandika Miquissone.

Miquissone tayari ameshathibitishwa kuuzwa na Uongozi wa Simba SC, akihusishwa kusajiliwa na Mabingwa wa Soka Barani Afrika Al Ahly ya Misri.

KIPA WA YANGA AGOMBEWA NA TIMU KIBAO ZINAZOSAKA SAINI YAKE JOTO LA MOROCCO LAWAFANYA YANGA KUBADILI ‘GIA ANGANI’…UONGOZI WAFUNGUKA HAYA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply