Home Yanga SC BREAKING: YANGA YAMTAMBULISHA NYOTA MPYA MWINGINE

BREAKING: YANGA YAMTAMBULISHA NYOTA MPYA MWINGINE


 UONGOZI wa Yanga leo umemtambulisha nyota mpya mwingine ambaye atakuwa ndani ya kikosi hicho kwa ajili ya msimu ujao wa 2021/21 ikiwa ni baada ya jana Agosti Mosi kumtambulisha mshambuliaji Fiston Mayele ambaye amepewa jezi namba 9.

Ni Yusuph Athuman kutoka Biashara United ambaye ametambulishwa leo rasmi kwa dili la miaka miwili kuitumikia timu hiyo.

Taarifa rasmi kupitia ukurasa wa Instagram wa Yanga imeeleza kuwa kwa sasa Yusuph Athuman ni njano na kijani.

Nyota huyu ni mshambuliaji ambaye yupo kwenye timu ya taifa ya Tanzania chini ya miaka 20.

SOMA NA HII  WAKATI CHAMA AKIWA HURU SASA...YANGA WAANZA KUPIGA DANADANA KUHUSU KUMSAJILI...NABI ATAJWA....