KIUNGO Khalid Aucho kwa sasa yupo ardhi ya Tanzania ikiwa ni kwa ajili ya kumalizana na mabosi wa Yanga wanaohitaji saini yake.
Kiungo huyo awali alikuwa anapigiwa hesabu na mabosi wa Simba ambao walikuwa wanahitaji kuipata saini yake.
Ameshawasili Tanzania kwa ajili ya kukamilisha mazungumzo na mabosi wa Yanga ikiwa mazungumzo yatakwenda sawa anaweza kupewa dili la miaka miwili.