KIKOSI cha Simba jana kilikwea pipa kuelekea Morocco kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya msimu wa 2021/22. Kocha Mkuu wa Simba Didier Gomes amesema kuwa ni jambo la msingi kwao kupata muda wa maandalizi.
Kuhusu nyota wapya ambao wamesajiliwa watapata muda wa maandalizi pamoja na kuwa sawa kwa ajili ya kuipambania timu hiyo.