news

EMMANUEL OKWI AIBUKA KWENYE SIMBA DAY…MASHABIKI WASHINDWA KUJIZUIA

admin September 19, 2021 12:46 pm


Mchezaji wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi ameibukia katika tamasha la Simba (Simba Day).

Okwi alifika uwanjani saa 7:50 mchana akiwa amevalia fulana nyeusi, miwani na jinsi.

Baada ya kufika uwanjani hapo akiwa katika jukwaa la VIP A, mashabiki walilipuka kwa shangwe na kuanza kumshangilia.

Kuna baadhi ya Mashabiki walimvalisha mpaka skafu shingoni kwake ambazo zilikuwa na rangi nyekundu na nyeupe.

Mashabiki wengine wengi wakinguata na kupiga nae picha huku wengine walishindwa kujizuia na kuendelea kumshangilia.

Okwi baada ya kupata mzuka huo mkubwa wa mashabiki wa Simba alikwenda mbele ya eneo la VIP A, na kuanza kuwapungia mkono kwa kuwasalimia.

BALOZI WA TANZANIA AKUTANA NA YANGA NIGERIA, KAZI IPO LEO SIMBA DAY  NI  KUFURUUUU…WAFUNGA TV KUBWA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6260

Leave a Reply