Uncategorized

ARSENAL WATEMBEZA KICHAPO CARABAO CUP

admin September 23, 2021 3:43 am

 


ARSENAL imeibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya AFC Wimbledon katika mchezo wa Carabao Cup ikiwa ni hatua ya raundi ya tatu.


Ni mabao ya Alexander Lacazette dakika ya 11 kwa mkwaju wa penalti na bao la pili lilipachikwa dakika ya 77 na Emile Smith Rowe lile la pili lilipachikwa na Eddie Nketiah dakika ya 80.


Arsenal ikiwa Uwanja wa Emirates iliweza kupiga jumla ya mashuti 19 na ni matano yalilenga lango na wapinzani wao walipiga mashuti manne na hawakuwa na shuti hata moja ambalo lililenga lango.

Umiliki wa mpira ilikuwa ni asilimia 63 kwa Arsenal na 37 kwa wapinzani wao.

EXCLUSIVE:SHABIKI WA YANGA AFUNGUKA NAMNA ALIVYOANZA KUIPENDA TIMU HIYO SAMUEL ETO’O KUWANIA URAIS

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply