Home kimataifa KLOPP ACHEKELEA MANE KUFIKISHA MABAO 100, ASEMA NI NAMBA TU

KLOPP ACHEKELEA MANE KUFIKISHA MABAO 100, ASEMA NI NAMBA TU


 KOCHA Mkuu wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema kuwa anafuraha kuona anamfundisha mshambuliaji mwenye uwezo Sadio Mane.

Raia huyo wa Senegal ni moja ya nyota ambao wana uhakika wa namba kikosi cha kwanza katika Ligi Kuu England ndani ya kikosi hicho.

Juzi alifanikiwa kufikisha jumla ya mabao 100 akiwa na Liverpool kwenye mchezo wa Ligi Kuu England dhidi Crystal Palace wakati timu hiyo iliposhinda kwa mabao 3-0.

Klopp amesema:”Hili ni jambo zuri sana na fahari kwangu kuona kuwa ninamfundisha mchezaji wa aina yake.

“Mabao 100 ni kama namba tu lakini ukweli ni kwamba ninafuraha sana kuwa naye,” amesema.

SOMA NA HII  FT:- YANGA 1-3 APR.....SIMBA NJIA NYEUPEEE....SHIBOUB AKUMBUSHIA ENZI....SKUDU CHALII...