MZEE wa Utopolo ambaye ni moja ya shabiki wa Yanga ameweka wazi kuwa matokeo ambayo wameyapata jana Septemba 12 kwa kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya Rivers United wanayapokea kwa kuwa hakuna ambacho kinaweza kubadilika na badala yake wanapaswa kubadili pale ambapo wamekosea huku wakiamini kwamba kwenye mchezo wa marudio unaotarajiwa kuchezwa nchini Nigeria watacheza tofauti na kupata matokeo chanya.