BAKARI Shime, Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Wanawake, ‘Twiga Stars’ amesema kuwa baada ya timu hiyo kupangiwa kucheza na timu ya taifa ya Zambia wamejipanga vizuri na wanaamini kwamba utakuwa ni mchezo mgumu.
Mchezo huo ni wa Hatua ya Nusu Fainali mashindano ya COSAFA yanayofanyika Port Elizabeth,Afrika Kusini.