Home news MO DEWJI AIAMBIA DUNIA KUHUSU SIMBA..ADAI ANAPOTEZA PESA NYINGI NA KUPATA HASARA

MO DEWJI AIAMBIA DUNIA KUHUSU SIMBA..ADAI ANAPOTEZA PESA NYINGI NA KUPATA HASARA


MFANYABIASHARA maarufu Tanzania na Afrika kwa ujumla ambaye pia ni mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohamed Dewji ‘Mo Dewji’ akihojiwa na Shirika la Utangazaji la CCN nchini Marekani  amesema amewekeza kwenye klabu ya (10) kwa ubora Barani Afrika na ina mashabiki  milioni 40.

Amesema pesa zake zinapotea kwani hapati faida, mpaka sasa ametumia zaidi ya dola za Kimarekani milioni 20 bila kupata faida, lakini amewekeza kutokana na mapenzi tu, lakini klabu hiyo haimuingizii faida yeyote.

“Simba SC ina miaka 85, ina mashabiki 40m, ndani ya miaka 4 nimewekeza dola milioni 20 ili iwe miongoni mwa klabu 10 bora Afrika. Tuna malengo makubwa. Hakuna biashara ila napoteza hela nyingi. Nafanya haya kwa mapenzi yangu sababu naipenda sana Simba,” amesema Mo Dewji.

Chanzo- Globalpublishers.co.tz

SOMA NA HII  KUELEKEA MECHI vs AL AHLY KESHO....DHAMIRA YA BENCHIKHA NA SIMBA IKO PALE PALE....