Home news SAA KADHAA KABLA YA KUSHUKA DIMBANI HUKO NIGER..BOCCO AIBUKA NA HILI JIPYA…AOMBA...

SAA KADHAA KABLA YA KUSHUKA DIMBANI HUKO NIGER..BOCCO AIBUKA NA HILI JIPYA…AOMBA DUA…


JOHN Bocco, Nahodha wa Simba, amesema hawatawaangusha Watanzania kwenye mashindano ya kimataifa kwa kuwa wapo vizuri na watapambana bila kuchoka.

Simba ikiwa Kundi D la michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, leo Jumapili inatarajiwa kutupa kete yake ya pili mbele ya US Gendarmerie, mechi ikichezwa nchini Niger.

Akizungumza na gazeti la Spoti Xtra, Bocco alisema: “Kwa upande wa ushindi hata wachezaji pia tunapenda na furaha yetu kuona inakuwa hivyo, tutapambana kufanya vizuri, hatutawaangusha Watanzania, kikubwa wao watuombee.” Katika mchezo dhidi ya ASEC Mimosas, Bocco alitoa pasi moja ya bao kwenye ushindi wa 3-1.

SOMA NA HII  PAMOJA NA SIMBA KUSHINDA JANA ...INJIA HERSI AVUNJA UKIMYA KUHUSU YANGA YAKE....ADAI BADO SANA ...