KOCHA wa Yanga, Nasreddine Nabi alikuwa miongoni mwa watazamaji wa mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba na RS Berkane.
Kocha huyo ambaye ameiongoza Yanga kuongoza ligi kwenye msimamo, ameonekana akiwa amevaa kofia nyeusi na shati jeupe na kukaa jukwa la VVIP.
Nabi amekuja kuangalia mchezo huo ambao ni wa kundi D Simba wakishuka dimbani wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kupoteza mchezo uliopita ugenini.
Pia hiyo ni fursa kwa Mtunisia huyo kuona namna gani mbavyo atawaandaa vijana wake kwa ajili ya mchezo wao wa ligi dhidi ya Simba mwezi ujao.