Home Habari za michezo KUELEKEA MECHI YA KESHO DHIDI YA DODOMA….YANGA WAPATA PIGO…. YANICK BANGALA NAYE...

KUELEKEA MECHI YA KESHO DHIDI YA DODOMA….YANGA WAPATA PIGO…. YANICK BANGALA NAYE ‘OUT’…


Yanga inatarajia kuwakosa Yacouba Sogne na Chico Ushindi kutokana na kuwa majeraha huku kiungo Yanick Bangala akiwa katika hati hati ya kucheza kutokana na kufiwa na Kaka yake.

Timu hiyo inatarajia kucheza kesho saa 10 jioni dhidi Dodoma mtanange unaotarajiwa kufanyika katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Kocha wa Yanga, Nesreddine Nabi amesema Yacouba amekuwa kwenye majeruhi kwa muda mrefu huku Chico bado hajapona vizuri.

Kuhusu Bangala amesema jana alipata taarifa ya msiba wa kufiwa na kaka yake hivyo watashauriana acheze ama la.

“Tutaongea nae tuone jinsi anavyojisikia maamuzi ya kumtumia yatatokana na kikao cha leo cha sisi na yeye akijisikia vizuri tunaweza tukamjumuisha kama hatajisikii tunatakiwa kumheshimu kwani tangu ameanza ligi ameonesha mfano mzuri,”amesema.

SOMA NA HII  KUTOKA MKUTANO MKUU: YANGA WAVUNA BILIONI 7 ....

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here