Home Uncategorized CR 7 ACHEKELEA USHINDANI WAKE NA MESSI

CR 7 ACHEKELEA USHINDANI WAKE NA MESSI


CRISTIANO Ronaldo, nyota anayekipiga Juventus amesema kuwa alikuwa anafurahia uwepo wake ndani ya Real Madrid kwa kupata ushindani mkubwa kwa mpinzani wake wa karibu Lionel Messi.

Cr 7 amesema kuwa alikuwa bora muda mrefu alipokuwa ndani ya Ligi Kuu ya Hisapania maarufu kama La Liga hata alipohama bado amekuwa akipambana kwa ajili ya kuendelea kuwa bora zaidi.

“Ni mchezaji ambaye uwezo wake ni mkubwa alikuwa ananipa changamoto nilipokuwa Hispania naona bado ananipa changamoto licha ya kwamba kwa sasa sipo ndani ya ligi ya Hispania,” amesema Cr 7 ambaye kwa sasa yupo ndani ya Ligi ya Serie A.

SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA NYUMA GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA