Kinara wa mabao wa Ligi kuu NBC ,George Mpole kutoka katika klabu ya Geita Gold amesema hayupo tayari kupambana na mchezaji yoyote wa ligi kuu na wala timu yoyote.
Akizungumza na waandishi wa habari George Mpole mara baada ya kuisaidia timu yake kupata alama moja dhidi ya Simba Mei 22 katika uwanja wa CCM Kirumba nakufikisha mabao 14 akifatiwa na straika wa Yanga Fiston Mayele mwenye mabao 13.
“ Mechi bado zipo nyingi hivyo mimi siwezi kuridhika bado tuna michezo mitano na tunazidi kupambana ili timu yetu ifikishe malengo tulijiweka kwa msimi huu”amesema George Mpole.
Vile vile Mpole ambae amewahi kuichezea Polisi Tanzania amesema ligi ya msimu huu imekuwa ni ngumu na yenyewe ushindani.