Home Habari za michezo KUELEKEA MASHINDANO YA CAF MSIMU UJAO…ISHU YA ITC ZA WACHEZAJI WAPYA ZAWASHTUA...

KUELEKEA MASHINDANO YA CAF MSIMU UJAO…ISHU YA ITC ZA WACHEZAJI WAPYA ZAWASHTUA YANGA…MANARA ANG’AKA…


Uongozi wa klabu ya Yanga, umeahidi kutorudia makosa katika michuano ya kimataifa kwa kujipanga vyema na kuhakikisha wachezaji wapya wanapata vibali mapema vitakavyowaruhusu kucheza michuano ya Klabu bingwani barano Afrika.

Yanga tayari imejihakikishia kucheza Ligi ya Mabingwa Afrika msimu ujao baada ya kufanikiwa kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Msimu uliopita, Yanga iliwakosa baadhi ya wachezaji wa kimataifa kutokana na kuchelewa kupata Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) akiwemo Khalid Aucho.

Akizungumza na waandishi wa habari Msemaji wa Yanga Haji Manara, amesema msimu uliopita timu yao ilishindwa kufanya vizuri baada ya wachezaji wao tegemeo kuchelewa kupata ITC.

”Tayari wamejifunza katika hilo, hiyo ndio sababu ya kukamilisha usajili wao wa wachezaji wapya mapema ili kuhakikisha wote wanakuwepo katika kikosi chao” amesema Haji Manara.

SOMA NA HII  BAADA YA CAF KUIPA SIMBA SC MASHABIKI...AHMED ALLY KAFIKIRIA WEEE..KISHA AKAIBUKA NA KAULI HII YA KIBABE...

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here