Home Habari za michezo KISA SIMBA…DJIGUI DIARA AWEKWA KANDO YANGA….NABI AFUNGUKA A-Z MAMBO YALIVYO…AMTAJA SAKHO….

KISA SIMBA…DJIGUI DIARA AWEKWA KANDO YANGA….NABI AFUNGUKA A-Z MAMBO YALIVYO…AMTAJA SAKHO….


Kocha wa wa Yanga Mohammed Nabi amesema kuna hati hati kama kipa wake Djigui Diarra anaweza kuwa seahemu ya mchezo huo kwani alipata majeraha katika mechi dhidi ya Simba SC, Jumamosi iliyopita.

Nabi ameyasema hayo leo Agosti 15, 2022 akiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar tayari kwa safari ya kwenda jijini Arusha kukabiliana na Polisi Tanzania katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu utakaopigwa kesho Agosti 16,2022.

Nabi alisema, Diarra aliumia katika mchezo huo wa Dabi baada ya kugongana na Pape Othman Sakho hivyo anatarajia kuzungumza na daktari kuona kama anaweza kufanya mazoezi na wenzake hii leo.

“Yupo pia Lomalisa (Joyce) na Diarra ambao wana injari. Diarra aligongana vibaya na Sakho katika mchezo uliopita hivyo tutaangalia daktari leo kama atasema yuko sawa kufanya mazoezi leo basi tutakuwa naye,” alisema Nabi.

SOMA NA HII  FT: SIMBA 0-0 COASTAL UNION....SIMBA WALALA DOROO...NA KADI NYEKUNDU JUU