Habari za michezo
SAMATTA AANZA KUKIWASHA UPYA NA TIMU YAKE YA GENK….APIGA ‘BONGE LA GOLI’ DAKIKA ZA JIONI…
Mshambuliaji Mbwana Samatta alifunga katika dakika ya nyongeza na kuisaidia KRC GENK kuibuka na ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya Royale Union Saint Gilloise kwenye ligi kuu soka nchini Ubelgiji.
Hili ni bao la kwanza kwa Samatta tangu arejee rasmi kwenye kikosi hicho kwa mkopo wa msimu mzima.
Ushindi huo umeifanya Genk kufikisha alama 19 katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi hiyo.
MATOKEO
Royale Union 1-2 KRC Genk
Wafungaji
⚽ 15′ Paintsil
⚽ 74′ Lapoussin
⚽ 90+2′ Mbwana Samatta

Leave a Reply
You must be logged in to post a comment.