BAADA ya kushindwa kupata bao ndani ya dakika 180 kinara wa mabao Simba, Moses Phiri amefunga bao lake la tano na kutoa pasi moja ya bao timu yake ikiibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Mtibwa Sugar mchezo wa Ligi Kuu NBC.
Mabao mawili ya Sakho, Okrah, Mzamiru na Phiri wakifunga moja moja yameipa Simba pointi tatu muhimu na kuishusha Mtibwa katika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo.
Simba imecheza mchezo dakika zote 90 wakionyesha ubora maeneo yote na uchu wa kufunga mabao zaidi pamoja na kufunga mabao dakika za mwanzo za mchezo.
Bao la kwanza la Simba liligungwa kipindi cha kwanza na Mzamiru Yassin dakika ya 38 akipokea pasi safi kutoka ya Okra bao ambalo lilidumu hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza.