Home Habari za michezo NTIBANZONKIZA AANZA MAJAMBOZI GEITA GOLD…SHIZA KICHUYA NAYE YUMO…

NTIBANZONKIZA AANZA MAJAMBOZI GEITA GOLD…SHIZA KICHUYA NAYE YUMO…

Timu ya Geita Gold imeibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jana Uwanja wa Nyankumbu mjini Geita.

Mabao ya Geita Gold yamefungwa na Said Ntibanzokiza kwa penalti dakika ya 18 na Offen Chikola dakika ya 53, wakati la Namungo FC limefungwa na Shiza Kichuya dakika ya 12.

Kwa matokeo hayo, Geita Gold inafikisha pointi 10 katika mchezo wa nane na kusogea nafasi ya tisa, wakati Namungo FC inabaki na pointi zake 11 za mechi saba nafasi ya saba.

SOMA NA HII  PAMOJA NA KUFUNGWA...MBRAZILI SIMBA AFUNGUKA ATAKAVYOITUMIA UGANDA KIMAFIA...