Tangu akiwa Azam FC kabla ya kutua Simba miaka ya nyuma aliwahi kushinda tuzo za kipa bora mara nne mfululizo kabla ya kusimamishwa na kipa wa Yanga, Djigui Diarra msimu uliopita.
Katika hilo walizungumza mara kwa mara na mabeki wake huku akiambiwa kuwa anatakiwa kuwa makini muda wote wa mchezo, hali inayompa kiwango kizuri kwa sasa. Nje ya Kepa wakati wa ujio wa David De Gea kwenye timu ya Manchester United 2011 moja ya tatizo alilokuwa nalo lilikuwa la kukosa nguvu ya mikono kucheza mipira inayopigwa kwa kasi kwenda golini kwake na kutoona kwa ukaribu likisababisha kufungwa mabao kirahisi.
Hii ni mbaya sana Simba. Haraka sana waendelee kuleta makocha wa makipa ili watibu changamoto alinayo Manula maana sasa Simba ni wakubwa kwa kiasi chake Afrika, hivyo klabu nyingi huifuatalia na zikiona zina faida ya kushinda mchezo kupitia eneo la kipa itakuwa njia rahisi kupata matokeo.