- Habari za michezo
- Habari za Yanga
- Habari za Yanga Leo
- Michezo
- Michezo Bongo
- Michezo Soka la Bongo
- news
- Yanga SC
Katika mechi ya juzi, Yanga haikuwa na mzuka kama ilivyokuwa dhidi ya Al Hilal ikiwa nyumbani, kwani nyota wake walionekana kuwa wachovu pengine kutokana na fatiki ya kucheza mechi mfululizo za Ligi Kuu Bara.
Winga Tuisila Kisinda alistahili kutolewa mapema katika mchezo huo ni bahati kwake kumaliza dakika 45 za kwanza kutokana na kutokuwa na jipya. Mtaji wake mkubwa ulikuwa ni mbio na hakukuwa na nafasi ya kufanikisha hilo kutokana na wapinzani wao hawakuwa na akili ya kushambulia kabisa na mabeki wao wa pembeni kuvuka hata nusu ya uwanja.
Katika mazingira magumu kama ambayo Yanga inapitia sasa, hasa katika kukosa matokeo bora lazima mtu wa kwanza kumulikwa ni kocha mkuu wa timu hiyo, Nasreddine Nabi kwa kuwa Yanga inategemea ubunifu wake katika kutengeneza mbinu za kupenya katika mazingira kama hayo.