Kwa pesa mpira wetu unazoingiza kutoka Azam Media. Kwa pesa mpira wetu unazoingiza kutoka SportPesa. Kwa pesa tunazoingiza kutoka M-Bet. Kwa pesa tunazoingiza kutoka kwa watu binafsi kama Said Bakhresa, Ghalib Said Mohammed, Mohammed Dewji na wengineo tulipaswa kuwa mbali sana.
Haya sio mafanikio yanayoenda na ukubwa wa timu zetu. Timu zetu ni kubwa. Timu zetu kuna pesa zinazalishwa. Timu zetu zina wadhamini wanamwaga pesa. Tuache kuridhika na vitu vidogo. Simba wanatakiwa kufika walau nusu fainali msimu huu ili mwakani mipango iwe ni kwenda kuchukuwa ubingwa.