Home Habari za michezo UKWELI MCHUNGU…SIMBA SC WASIPOJIANGALIA KATIKA HAYA…HATA HUKO KIMATAIFA WASAHAU…
- Habari za michezo
- Habari za Simba
- Habari za Simba Leo
- Michezo
- Michezo Bongo
- Michezo Soka la Bongo
- news
- Simba SC
Simba kutinga makundi sio kitu chenye presha kwao kwa sababu kuna wachezaji wengi ambao wameishi katika mechi hizo kubwa na wala haikuwa kitu kigumu kwao hasa walipokutana na timu changa kama Nyassa Big Bullets ya Malawi na hata Primeiro de Agosto ya Angola.
Wakati wa dirisha la usajili Simba ilipiga hesabu rahisi kwa kuwasajili washambuliaji Habib Kyombo, Dejan Georgijevic, viungo, Victor Akpan, Nelson Okwa, haukuwa usajili ambao umeibeba ni sawa na kusema matarajio yao yalishindwa kufikiwa.
Wapo wachezaji wanaoonekana umri kuwatupa mkono, hili nalo sio jipya, Simba waliangalie kwa kina kama wataona mchango mdogo kwa wachezaji ambao waliwapa mafanikio hata kama ni wazawa waachane nao kwa heshima kama walivyofanya kwa Meddie Kagere na hata Thadeo Lwanga.
Usajili uliopita Simba ilisajili kwa papara na kukosa uwiano wa ushindani wa mchezaji kwa mfano viungo wakabaji ndani ya kikosi hicho anza na Akpan, Jonas Mkude, Nassoro Kapama, Mzamiru Yassin na Sadio Kanoute. Kwenye lundo la viungo wakabaji watano utaona hesabu za usajili hazikufanyika kitataalam hakuna hata mmoja ambaye angeweza kucheza kama kiungo mshambuliaji wa juu na akafanya kitu kikubwa.
Mbele ndio kuna mashaka zaidi tegemezi limebaki kwa Phiri na Augustine Okrah kidogo, ndio wamekuwa wakifunika udhaifu wa wengine. Katiuka mechi tano zilizopita Phiri amefunga mabao matano, akishindwa kufunga dhidi ya Yanga, Azam, Singida Big Stars na Ihefu huku akifunga dhidi ya Mtibwa.
Simba inatakiwa kurudi sokoni kutafuta wafungaji wenye ubora kazi ambayo haihitaji kukurupuka watangulize utulivu ni bora wakate lundo la wachezaji wa kawaida kisha wakatumie bajeti inayokidhi soko kuwapata watu bora wa ufungaji kuirudishia timu hadhi yake uwanjani. Ili kutinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika inahitaji wachezaji wa kutembeza boli na kutupia.
Kufika hatua hii Simba ya Ligi ya Mabingwa Afrika inahitaji kuwa na malengo kama hayo lakini kwa ubora wa kikosi chao utagundua hakina uhalisia wa kufika huko kama tu kilishindwa hata kupata pointi mbili katika mechi za kikubwa dhidi ya Azam, Yanga na Singida.