Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.

Kifupi ni kwamba hawapo katika kiwango cha kucheza katika Kombe la Dunia. Kilichosababisha wacheze ni kwa sababu wao ni waandaaji wa michuano hii. Hata unapopiga hesabu ya wao kufuzu kama wasingekuwa waandaaji bado haoni wangeweza kufuzu vipi mbele ya Australia, Japan na Korea Kusini.
Mastaa wao wakiongozwa na staa Akram Afif ambaye ni mtoto wa staa wa zamani wa Simba, Hassan Afif wote wanacheza nyumbani. Wamejifungia nyumbani kwahiyo huwa wanajidanganya kwa viwango vyao wenyewe. Hili ndilo tatizo ambalo hata Tanzania na timu yetu ya taifa tunalo.
Ambacho Qatar walipaswa kukumbuka katika soka la kisasa ni kuwapeleka mastaa wao wakapate uzoefu wa kucheza nje. Walau mastaa wao wangeenda kucheza katika timu za kawaida Ulaya wangeweza kupata hisia za upinzani katika soka halisi.
Hakuna kitakachobadilika pindi watakapocheza na Senegal kisha Uholanzi. Wote hawa wawili wapo katika viwango vya ushindani wa kimataifa. Senegal imejaza mastaa wanaocheza Ulaya kama ambavyo ilivyo kwa Uholanzi. Ni ngumu kwa Qatar kufanya chochote labda miujiza ya Mungu itumike.

