Home Habari za michezo SAKATA LA KUJIUZULU BARBARA…MENGINE MAPYA YAIBUKA…ALIKUWA HAZIIVI NA ‘TRY AGAIN’….
- Habari za michezo
- Habari za Simba
- Habari za Simba Leo
- Michezo
- Michezo Bongo
- Michezo Soka la Bongo
- news
- Simba SC
Inaelezwa sababu ya kwanza iliyochangia kwa Barbara kufanya uamuzi wa kuondoka Simba ni kushindwa kuelewana vizuri na mabosi wake wakiwamo Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi.
Katika kipindi cha miaka miwili Barbara alichokuwa ndani ya Simba alionekana kuwa kiongozi mwenye malengo ya kuhakikisha mdhamini, Mo Dewji anatoa kiasi kidogo cha pesa kwenye uendeshaji wa timu huku akipunguza baadhi ya matumizi kwenye maeneo mengi.
Kati ya mambo makubwa yaliyochangia Barbara kuondoka ndani ya Simba ni hili, kwa kipindi kirefu sasa hakuna maelewano mazuri kati yake na bosi wake, Salim Abdallah ‘Try Again’. Try Again aliteuliwa katika nafasi hiyo baada ya Mo Dewji kujiondoa ili kubaki kuwa Rais wa Heshima wa klabu hiyo.
Miaka minne iliyopita Simba ilifanya vizuri katika mashindano ya kimataifa na ndani ikiwemo kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Bara kwenye misimu hiyo mfululizo.
Huku nje, wapenzi na mashabiki wa Simba wengi wao walikuwa huwambii kitu kuhusu Barbara wakiamini ni kati ya viongozi wanaofanya kazi yao nzuri ndani ya klabu kwa muda wote.