Wakati mazungumzo yakiendelea kuhusiana na hatma ya mkataba kati ya Yanga na mdhamini wao SportPesa,
Rais wa klabu hio Hersi Said amekiri kuwa baadhi ya vipengele vilivyokuwa vinaibana Yanga wamevikiuka katika mkataba wake na SportPesa.
Akihojiwa na kituo cha Television cha Clouds, Hersi amesema kuwa baada ya kuingia mkataba mpya na kampuni ya Haier, baadhi ya vipengele ambavyo Klabu wanatakiwa kuendelea kuvitekeleza ni pamoja na kuvaa kits za SportPesa katika mazoezi au wakati wanasafiri, kuiweka logo ya SportPesa katika banners wakati wa press conference na katika mawasiliano ya social media.
Hata hivyo ushahidi upo unaoonyesha kuwa toka waingie mkataba na kampuni ya Haier, Yanga wamekuwa hawatimizi mahitaji hayo ya mkataba.