WACHEZAJI TP MAZEMBE WAKATWA MISHAHARA...KWA KUSHINDWA KUVUKA MAKUNDI
Habari za michezo

WACHEZAJI TP MAZEMBE WAKATWA MISHAHARA…KWA KUSHINDWA KUVUKA MAKUNDI

Marce Ben Komba March 20, 2023 3:48 pm

Asiyefanya kazi na asile. Ndicho ambacho Bilionea Moise Katumbi ameamua kwa mastaa wake, watakatwa mishahara yao kwa asilimia 25 kwa Kushindwa kuvuka hatua ya Makundi katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Roho mbaya hii sio ya ghafla ghafla tu. hivi ndivyo ilivyo kwa katika mpangilio wa mishahara ya mastaa wa Mazembe kwa mujibu wa mikataba yao.

Watalazimika kukatwa robo ya mishahara yao kama wakishindwa kuivusha Makundi timu yao katika michuano ya Afrika, na jana rasmi wamejitoa katika kinyanganyiro cha kufuzu kwa hatua ya Robo Fainali Kombe la Shirikisho Afrika baada ya kukubali kichapo cha magoli 2-1 mbele ya Real Bamako.

AZAM FC HII SASA KOMOA…WAJITAYARISHA KUIVAA GOR MAHIA BARBARA ATOBOA SIRI…USAJILI WA ADEBAYO KUTUA SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply