BAADA ya Yanga Princess kuonekana kusuasua kwenye Ligi ya Wanawake (WPL) msimu huu hatimaye viongozi wamefikia makubaliano ya pande zote mbili kuvunja mkataba na Kocha huyo.
Taarifa iliyotolewa leo na Ofisi ya Mtendaji Mkuu wa Yanga imeeleza kuwa kikosi hicho kwasasa kipo chini ya Kocha Fredy Mbuna mpaka pale msimu utakapomalizika huku sababu za kuvunja mkataba huo zikiwa hazijawekwa wazi.
“Uongozi wa Klabu ya Yanga unapenda kuutaarifu umma kuwa umefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na Kocha Mkuu wa Timu ya Wanawake, Yanga Princess, Sebastian Nkoma”.