Mechi za hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika zimekamilika usiku wa kuamkia leo ambapo timu zote zilizofuzu katika hatua hiyo zimefahamika
Al Ahly imekamilisha hesabu ya timu nane zilizotinga robo fainali baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Al Hilal
Kutoka kundi A, Wydad Casablanca na JS Kabylie zimetinga robo fainali huku Wydad wakiwa vinara wa kundi
Kundi B ni Mamelodi Sundowns na Al Ahly, Mamelodi wakiwa vinara wa kundi
Kundi C ni Raja Casablanca na Simba wakati kundi D ni Esperance na CR Belouizdad vinara wa kundi wakiwa ni Esperance