MECHI HII YA YANGA YAPELEKWA MBELE...HUYO NABI SASA!!
Habari za michezo

MECHI HII YA YANGA YAPELEKWA MBELE…HUYO NABI SASA!!

Marce Ben Komba April 19, 2023 9:04 am

Bodi ya Ligi Kuu itaupangia tarehe nyingine mchezo wa ligi kuu kati ya Singida BS dhidi ya Yanga ambao ulipaswa kupigwa mwishoni mwa wiki
Yanga inatarajiwa kusafiri nchini Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Rivers United utakaopigwa Jumapili April 23

Mchezo wa marudiano utapigwa April 30 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Baada ya Singida BS, mchezo utakaofuata ni dhidi ya Dodoma Jiji ambao utapigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi

Ratiba ya mchezo huo nayo huenda ikaathiriwa kutokana na ratiba ta mechi za CAF

Yanga itakwenda kuhitimisha msimu mkoani Mbeya kwa mechi mbili dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons

Katika mechi nne zilizosalia, Yanga inahitaji alama nane ili kitetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

Wananchi pia wanakabiliwa na mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Singida BS ambao utapigwa uwanja wa Liti, Singida

NI SIMBA SC TENA….CAF KUTUMA WATAALAMU KUJA KUFANIKISHA JAMBO MECHI NA WYDAD… KOCHA SIMBA AFICHUA SIRI HII YA KUIBANJUA YANGA…AMEFUNGUKA HAYA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply