Home news BAADA YA KUTUNGULIWA KIMOJA DAR…WYDAD WAAMUA KUFANYA MAAMUZI HAYA MAZITO…

BAADA YA KUTUNGULIWA KIMOJA DAR…WYDAD WAAMUA KUFANYA MAAMUZI HAYA MAZITO…

Simba vs Wydad

KOCHA mkuu wa Wydad Casablanca, Juan Carlos Garrido amesema licha ya matokeo waliyoyapata dhidi ya Simba SC, bado wana mchezo mwingine wa kujitetea wakiwa nyumbani.

Wydad imefungwa 1-0 na Simba SC bao lililowekwa wavuni na Jean Baleke mchezo uliochezwa juzi Uwanja wa Mkapa.

Akizungumza baada ya mchezo, Garrido alisema walipambana vya kutosha lakini hawakutumia vizuri nafasi walizopata na sasa nguvu wanahamishia mechi inayofuata.

“Tutafanya uchambuzi wa mechi hii ili kuhakikisha kwenye mechi ijayo tunapata matokeo mazuri;

“Tumecheza kipindi cha kwanza hapa ugenini na tunakwenda nyumbani kucheza kipindi cha pili tuna imani tutafuzu hatua inayofuata.”

Garrido amesema watakuwa na hali nzuri kwenye mchezo wa marudiano kuhakikisha wanatumia vizuri nafasi.

“Tulikuwa na nafasi nyingi nzuri za kufunga kwenye kipindi cha kwanza lakini haikuwa hivyo, wenzetu wametumia nafasi waliyopata.

“Hali ya hewa ya kucheza saa 10 jioni sio rafiki sana kwetu japokuwa imechangia kwa kiasi chake lakini isiwe sababu, tunajiandaa kwa ajili ya mchezo ujao.” Wydad na Simba zitarudiana Aprili 28 nchini Morocco.

SOMA NA HII  BALOZI WA UINGEREZA ALIVYOWAPA MAUJANJA SIMBA LEO...AHADI YAKE KUBWA NI HII HAPA...