Home Habari za michezo EDO KUMWEMBE AFURAHI YANGA SC KUFUNGWA NA SIMBA ….:”ILIBIDI WAFUNGWE GOLI 4-0″…

EDO KUMWEMBE AFURAHI YANGA SC KUFUNGWA NA SIMBA ….:”ILIBIDI WAFUNGWE GOLI 4-0″…

Habari za Yanga SC

Wakati Mchezo wa Watani wa jadi kati ya Simba na Yanga ukitamatika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 na kufuta uteja mbele ya Yanga wa kutoshinda kwa miaka 3.

Mchambuzi wa Michezo kutoka kituo cha Wasafi FM, Edo Kumwembe yeye anasema amefurahi Yanga kupoteza mchezo huo.

Akifafanua Edo anasema;

“Mimi nimefurahi Yanga kufungwa, naamini Yanga angeshinda isingekuwa story kubwa kama ilivyo sasa kwa Simba kwa sababu wameifunga sana Simba siku za hivi karibuni.. Simba kushinda kutaongeza mvuto wa derby, Inawezekana tukaishuhudia derby nyingine ya Simba na Yanga msimu huu kwenye Kombe la (FA)”

“Yanga hawakuwa wamejiandaa na mechi, waliona kama wameshashinda mechi kiurahisi na sio tu kwamba watashinda, watafunga mabao mengi. Simba walikuwa kimya wiki nzima, kuna jambo lao walikuwa wanaliwinda”

“Kwanza nimemshangaa sana Kocha Nabi kumlalamikia mwamuzi, Hadi Half time Yanga ilibidi wapigwe bao 4.

SOMA NA HII  HALI YA BOCCO YAZIDI KUSIKITISHA SIMBA...KACHEZA MECHI 14 BILA KUCHEKA..