Home Habari za michezo KISA YANGA SC KUNUSA NUSU FAINAL CAF…ALLY KAMWE AMPIGA KIJEMBE HIKI MO...

KISA YANGA SC KUNUSA NUSU FAINAL CAF…ALLY KAMWE AMPIGA KIJEMBE HIKI MO DEWJI…

Habari za Yanga SC

Wakati Yanga SC wakiwa tayari wameshatanguliza mguu mmoja Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Rivers United ya Nigeria.

Tayari Afisa Habari wa Yanga ameshaanza mbwembwe na kutupa vijembe kwa watani zao Simba SC.

Akizungumza kupitia kipindi cha Sports Arena ally Kamwe anasema;

“Ghalib ni Bilionea ambaye amewekeza kwa muda mfupi na timu inakaribia kwenda nusu fainali, kuna watu wamewekeza pesa, masimango, vichambo, minuno na kila aina ya gubu na wanaishia robo fainali,”

Simba na Yanga wote kwa pamoja wanasubiri michezo ya Mkondo wa pili kujihakikishia kutinga hatua ya Nusu Fainali Michuano ya CAF.

SOMA NA HII  SAA KADHAA KABLA YA MECHI NA WASAUZI LEO....YANGA WAIVIMBIA CAF....WADAI KUNA HILA...