Home Habari za michezo KUELEKEA MECHI NA WAARABU…KITENGE ASHINDWA KUJIZUIA…AWAPA UJUMBE HUU SIMBA SC….

KUELEKEA MECHI NA WAARABU…KITENGE ASHINDWA KUJIZUIA…AWAPA UJUMBE HUU SIMBA SC….

Habari za Simba SC

Wakati Simba SC wakikutana na kila aina ya vitisho kuelekea mchezo wao wa marudiano ugenini dhidi ya Wydad Casablanca.

Mwandishi wa Michezo Mkongwe, Maulid Kitenge nae ametoa rai yake kwa Simba SC kuelekea mchezo huo.

Akizungumza Maulid anasema;

“Casablanca ni mji wa wapenda mpira na wanazipenda timu zao, kwa hiyo moja Ya vitu ambayo Simba watakutana navyo ni ile Atmosphere ya uwanjani kwanza inakuchanganya.

“Taifa hapa walikuwa wachache wakawasha kama ‘kimoto’ hivi sasa ile ndo inakuwa uwanja mzima unalipuka.

“Mimi niwaambie Simba, wasitishike na hali ambayo watakutana nayo, vitimbi vitakuwa vingi lakini focus yao ibaki katika dakika 90.

“Wana mtaji wa bao 1 wanahitaji sare, wapambane wasifunguke sana, wacheze kwa kuheshimu wapinzani na wajue wako ugenini, wasiruhusu goli la mapema,”

SOMA NA HII  MZAMIRU :- HAKUNA WAKUTUSIMAMISHA KWA TIMU ZA TANZANIA