Baadhi ya Wanahabari na Wachambuzi wa Soka nchini wamemtaka Afisa Habari wa klabu ya Simba, Ahmed Ally kuomba radhi kufuatia kauli yake aliyoitoa dhidi ya Yanga kuelekea mchezo wa Dabi Jumapili hii.
Katika mazungumzo na Wanahabari Ahmed alisema;
“Yanga ni kama maiti hivyo wanakwenda kuwakamua” kauli hiyo imevuka mipaka ya utani wa jadi na ni kinyume na ueledi na ni tusi baya.