Tetesi za usajili Simba
Habari za michezo

MBADALA WA ONYANGO SIMBA HUYU HAPA….JAMAA ANAKABA MPAKA PUMZI AISEE…

admin May 24, 2023 10:43 am

Simba ipo katika harakati za kusuka upya kikosi chake na sasa imetua kwa beki na nahodha msaidizi wa timu ya taifa ya Rwanda Thierry Manzi ambaye kwa sasa yupo nchini Ubelgiji.

Manzi ni beki wa kati anayemudu kucheza namba nne na tano akitumia vyema miguu yote kwa ufasaha na anasifika kwa kukaba, kuanzisha mashambulizi na ni mkali wa kucheza mipira ya juu.

Kuelekeaa msimu ujao wekundu wa msimbazi Simba wamedhaamiria kufanya maboresho makubwa kwenye kikosi chao huku ikisadikiwa kuwa kuna namba kubwa ya mastaa wataingia.

Hata hivyo pia baadhi ya mastaa pia wanatajajwa kuwa watapigwa panga ili kupisha ujio wa mastaa wapya huku wachezaji wengi wa ndani wakitazamaiwa kukumbwa na panga hilo.

Baadhi ya mastaa ambao huenda wakapigwa panga ni pamoja na Jonas Mkude, Okrah, Banda, Sawadogo, huku wengine wakiwekwa kwenye mchujo.

Hawa ni baadhi ya Wachezaji ambao wanapambiwa na klabu ya Simba ili kuzipata saini zao kwenye dirisha lijalo la uhamisho.

Zougrana Mohamed

Harvy Ossete

Richard Boadu

Morice Chukwu

Gatoch Panom

HAYA HAPA MAJEMBE SABA YA SIMBA YA UHAKIKA…MABOSI WAKENUA MENO…. MAKAMBO NA YACOUBA KUTIKISA TENA LIGI YA BONGO…MAMBO YAPIGWA KIMYA KIMYA AISEE..

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply