Yanga ikiendeleza ‘Thank You’ jana imeachana na winga Dickson Ambundo ikiwa inafumua kikosi kwa ajili ya msimu ujao.
Ambundo amewaaga Wananchi na kwa kutoa ujumbe wenye hisia kupitia akaunti yake ya Instagram akiandika;
“Moja kati ya nyumba bora sana, nyumba yenye upendo, furaha, matumaini na umoja wa hali ya juu, nyumba ya mafunzo yanayotoa mwanga mzuri kwenye safari ya maisha, kwa huzuni leo nawaaga wenzangu kwenye nyumba lakini moyo wangu umejawa na shukrani za dhati kabisa kwa wenye nyumba kuanzia uongozi bora kabisa chini ya Rais Hersi Said, benchi la ufundi chini ya Nasreddine Nabi, wachezaji wenzangu na wananchi wote kwa ujumla.