Habari za Yanga
Habari za michezo

YANGA WAIPA SIMBA UTARATIBU HUU WA KUMUAGA MKUDE UWANJANI….

admin July 16, 2023 5:04 pm

Klabu ya Yanga imesema kuwa iwapo watani zao Simba wanataka kumuaga kwa heshima aliyekuwa mchezaji wao, Jonas Mkude basi wajitokeze Siku ya Mwananchi, Julai 22, 2023 katika Dimba la Mkapa.

Hayo yamesemwa na Ofisa Habari Yanga, Ally Kamwe baada ya klabu ya Yanga kumsajili kiungo huyo aliyedumu Simba kwa miaka 13.

“Kama wanataka kumuona au kumuaga Mkude kwa mara ya mwisho, mahali pekee wanapoweza kuja kumuona ni kwenye kilele ya Wiki ya Mwananchi.

“Kwa hiyo kama wanataka kumuaga tunawakaribisha waje siku ya Jumamosi Julai 22, 2023 tutawapa nafasi ya kusimama na kumgia hizo salute na parade halafu tutawaruhusu watoke waende kuendelea na shughuli nyingine.

“Mkude yupo kwa ajili ya Yanga na kuwapa furaha wanayanga, ataonekana siku ya kilele cha Wiki ya Mwananchi pekee.

“Wengine labda wanaweza kuongea na mamlaka za wanyama pori wakamchukua Nungunungu mwingine wakampeleka kwenye tamasha lao lakini Nungunungu kwa maana ya Jonas Mkude kama wanataka kumuaga waje siku ya kilele cha Wiki ya Mwananchi, tunawakaribisha,” amesema Ally Kamwe.

MAYELE APEWA RUHUSU RASMI NA YANGA, HUYU HAPA NDIO MRITHI WAKE WAKATI YANGA WAKIKUBALI YAISHE KWA MAYELE…..KIFAA KIPYA KITAKACHOMRITHI HIKI HAPA…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply