Habari za Yanga
Habari za michezo

SKUDU NA SAKATA LA JEZI YA FEI TOTO YANGA

Staff Desk July 21, 2023 9:08 pm

Nyota mpya wa Yanga,Mahlatse Makudubela’Skudu’ amesema hakuchagua kutumia jezi namba sita bali alichaguliwa.

Skudu amezungumza hayo leo muda mfupi kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kueleza kuwa hakuwahi kuivaa jezi namba sita kwenye timu yoyote.

Aidha alisema haikuwa rahisi kuchagua namba sita ambayo ilikuwa na kitendawili na presha kubwa.

“ Sikuichagua namba sita ila klabu ndio imenichagulia kabla ya Yanga sijawahi kuvaa jezi namba hiyo nilikiwa navaa namba 11 waliniambia wangependa kunipa jezi namba sita na nilisema ni heshima kwasababu niliona presha ya jezi hiyo na kila mtu anakuwa kulingana na presha” amesema Skudu

Skudu alitambulishwa Julai 18 na kupewa jezi namba 6 ambayo iliachwa wazi na kiungo wa zamani wa Yanga Feisal Salum ‘Fei Toto’ aliyeuzwa Azam FC.

Skudu amewahi kucheza Timu mbalimbali zikiwemo Mamelod Sundowns, Orlando Pirates, Highland Park na Chippa United zote za Afrika Kusini.

MTEGO WA MAYELE YANGA SASA HADHARANI MSHAHARA WA LUIS MIQUISSONE SIMBA KUFURU

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply