Sign in
  • Home
  • TAIFA STARS
  • SIMBA SC
  • YANGA SC
  • AZAM FC
  • KIMATAIFA
  • BURUDANI
Sign in
Welcome!Log into your account
Forgot your password?
Password recovery
Recover your password
Search
  • Sign in / Join
  • Blog
  • Forums
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.
  • Home
  • TAIFA STARS
  • SIMBA SC
  • YANGA SC
  • AZAM FC
  • KIMATAIFA
  • BURUDANI
Home Habari za michezo KIPA MBRAZIL WA SIMBA ATAKIWA KUTHIBITISHA UBORA WAKE, KIPA WA MAKOCHA AFUNGUKA...
  • Habari za michezo
  • Habari za Simba
  • Habari za Simba Leo
  • Michezo
  • Michezo Bongo
  • Michezo Soka la Bongo
  • news
  • Simba SC

KIPA MBRAZIL WA SIMBA ATAKIWA KUTHIBITISHA UBORA WAKE, KIPA WA MAKOCHA AFUNGUKA KILA KITU, MANULA ATAJWA

By
Staff Desk
-
July 29, 2023
2767
0
kipa wa simba

KIPA wa zamani na kocha wa makipa, Ivo Mapunda amesema kipa mpya wa Simba, Jefferson Luis Szerban anatakiwa kuthibitisha ubora wake kwani ameingia kwenye timu ambayo ina kipa namba moja wa timu ya Taifa, Aishi Manula.

Simba imemsajili kipa huyo raia wa Brazil kwa mkataba wa miaka miwili, kipindi hiki ndiye atakuwa akisimama langoni kwani Manula anauguza majeraha yake na atakuwa nje ya uwanja kwa miezi mitatu.

Akizungumza na Mwandishi, Ivo ambaye aliwahi kuzidakia Yanga, Simba, Azam FC na Taifa Stars alisema anaamini Manula atakapopona atarudi kwenye ubora wake na ndiye kipa namba moja wa Simba.

“Wote wana changamoto, ni ngumu sana kupambana na kipa namba moja wa timu ya Taifa, inawezekana ni kipa mzuri ila anapaswa kufanya kazi kubwa kuhakikisha anawapa Simba kile walichokitarajia na kinachozidi ubora wa Manula.

“Sio kila mchezaji wa kigeni anayesajiliwa anakuwa na uwezo wa kucheza, Luis ametoka kwenye nchi ambayo soka limezaliwa huko, tunapenda kuona tofauti yake kwa kiwango kikubwa,” alisema Ivo.

Ivo alisitiza anamfahamu Manula hata kama ana mapungufu ambayo hayamfanyi kutokuwa namba moja ndani ya Simba upande wa makipa.

“Kuuguza majeraha kuna mwisho na ninavyomfahamu Manula hawezi kukubali kupoteza namba kwa sababu tu ametoka kwenye majeraha, ni kipa mpambanaji, namba yake iko wazi kabisa pale Simba. Urefu wa Mbrazili huyo anaweza akawa mzuri mipira ya juu pengine hata ya chini, hii haizuii ila atuonyeshe ubora wake wa kumzidi mzawa.”

Simba imemsajili kipa huyo kutoka Resende FC ya Brazil na msimu uliopita ameichezea Itabirito FC-MG kwa mkopo na yupo kambini Uturuki.

Kwa usajili huo Simba inakuwa na makipa wanne Manula, Ally Salim, Ahmed Feruzi ‘Teru’ pamoja na Jefferson.

  • TAGS
  • Air manula
  • aishi manula
  • Habari za Michezo
  • kipa mbrazil wa simba
  • Mapunda
  • soka
  • soka la bongo
Previous articleWAWAKILISHI WA KOMBE LA SHIRIKISHO AFRIKA, SIMBA, YANGA, AZAM, SINGIDA FG, RATIBA KAMILI IKO HIVI
Next articleBANGALA AFUNGUKA MAZITO KABLA YA KUSEPA, HUYO MRITHI WA MAYELE ANAMTIHANI HUU HAPO YANGA
Staff Desk
Staff Desk

RELATED ARTICLESMORE FROM AUTHOR

YANGA KUNGIA KAMBINI DESEMBA 15

SIMBA HAIJAPOTEZA DIRA YAKE, AHMEDY ALLY

PEDRO AUWASHA MOTO YANGA, AKABIDHI RIPOTI NZITO

LEAVE A REPLY

Log in to leave a comment

329,001FansLike
12,344FollowersFollow
16,900SubscribersSubscribe
FcTables.com

EDITOR PICKS

RASMI YANGA YAMALIZANA NA MBUKINAFASO

admin - August 11, 2020

PHIRI, BALEKE ‘WAWEKEWA PANGA SHINGONI’…BENCHEKH AWAKATAA HADHARANI…MANGUNGO ATIA NENO..

admin - January 16, 2024

MUONEKANO WA UKURASA WA NYUMA GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA

admin - October 8, 2021

MIEZI KADHAA TOKA ATOKE SIMBA..SASA TUMEUONA UWEZO HALISI WA NDEMLA..NI WA KAWIDA MNOOO…

admin - January 25, 2022

EVEN MORE NEWS

YANGA KUNGIA KAMBINI DESEMBA 15

December 10, 2025

SIMBA HAIJAPOTEZA DIRA YAKE, AHMEDY ALLY

December 10, 2025

PEDRO AUWASHA MOTO YANGA, AKABIDHI RIPOTI NZITO

December 10, 2025

POPULAR CATEGORY

  • news12198
  • Michezo10204
  • Michezo Bongo10180
  • Habari za michezo10106
  • Michezo Soka la Bongo10035
  • Simba SC6317
  • Disclaimer
  • Privacy
  • Advertisement
  • Contact Us
©