Home Habari za michezo KIBEGI CHA SIMBA SC KIMESHAFIKA KILIMANJARO, UZI HUU HAPA

KIBEGI CHA SIMBA SC KIMESHAFIKA KILIMANJARO, UZI HUU HAPA

HATIMAE ile safari ya Kibegi cha Simba imegotea kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro.
Huu ni uzinduzi wa kwanza kwa Simba kufanya jambo hili kwa kuzindua uzi mpya kwenye mlima mrefu Afrika.

Ikumbukwe kwamba Simba ni mabalozi wa utalii wa ndani na kwenye mechi za kimataifa wana uzi wao wenye nembo ‘Visit Tanzania’.
Ni watu maalumu ambao ni mashabiki wa Simba wamefanikisha zoezi hili ikiwa ni maandalizi ya msimu wa 2023/24.

Uzi huo unapatikana kwenye maduka yote Tanzania na popote anayehitaji uzi mpya anapelekewa.

SOMA NA HII  AZIZ KI AWAGUMZO SOKA LA BONGO, ISHU NZIMA IKO HIVI