Habari za Yanga
news

YANGA :- SIMBA WAMEMKOSEA HESHIMA MANGUNGU….KWA NINI HAKUKAA NA RAIS SAMIA..?

admin August 10, 2023 2:09 pm

Jumapili iliyopita Simba walikuwa na Tamasha lao la “Simba Day” katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Kilele cha Tamasha hilo kilifana sana huku Simba wakipongezwa na wadau mbalimbali wa soak kwa namna walivyofanikisha Tamasha hilo.

Mgeni Rasmi katika Tamsha hilo alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.

Miongoni wa watu waliotoa pongezi zao ni Mkurugenzi wa Sheria wa Yanga wakili Simon Patrick ambae kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan alinogesha sherehe yenu watani hongereni, ila siku nyingine rekebisheni protocol, Mwenyekiti wa Klabu Mzee Mangungu sio wa kukaa VIP A, alipashwa akae hapo na mgeni rasmi kwani yeye ndio Kiongozi wa juu kwenye Klabu.

Je unakubaliana na kauli na ushauri huo wa Wakili Simon Patrick? Tupe maoni yako

BAADA YA JANA KUUMIA DK YA 6 TU…..HALI YA SKUDU IKO HIVI…YANGA WAVUNJA UKIMYA… KUMBE HIKI NDIO KINACHOWAPA JEURI SIMBA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply