habari za yanga
Habari za michezo

VITA YA NAMBA HUKO YANGA SASA IMESHAKUWA MAJANGA…… WAZAWA WAGOMA

Staff Desk August 13, 2023 11:33 am

Kuna vita kubwa ya namba ya namba inayoendelea kambini Yanga ni baada ya wachezaji wazawa kugoma kukaa benchi.

Yanga wapo kambini hivi sasa wakijiandaa na mchezo wa Ngai ya Jamii hatua ya fainali watakaocheza dhidi ya Simba SC Jumapili hii saa moja usiku.

Katika mchezo huo Yanga itawachezesha wachezaji wake wapya ambao imewasajili akiwemo Maxi Zangeli, Pacome Zouzoua, Attohoula Yao na Skudu Makudubele.

Meneja wa timu ya Yanga Walter Harrison alisema kuwa upo ushindani mkubwa wa namba hivi sasa katika kikosi hicho kati ya wachezaji wazawa na kigeni.

Walter alisema kuwa ushindani umetokana na ujio wa Kocha mpya Miguel Gamondi, kila mchezaji kupambana kumshawishi kocha ili aingie katika kikosi hicho.

Aliongeza kuwa wachezaji ambao hawakuwa sehemu ya kikosi cha kwanza katika msimu uliopita baadhi Denis Nkane na Chrispin Ngushi nao wameonyesha ushindani mkubwa .

“Ninaamini msimu huu kazi itakuwepo ya kushindania namba katika kikosi cha kwanza kutokana na kila mchezaji kutaka kuwepo sehemu ya kikosi cha kwanza.

” Wale wachezaji wa zamani ambao msimu uliopita ndio wamefanya ushindani uwe mkubwa, kwani wanaamini watapata nafasi ya kucheza kutokana na ujio wa kocha mpya.

“Gamondi ana kibarua kigumu katika msimu ujao kwenye kupanga kikosi, kwani kila mmoja yupo katika kiwango bora,” alisema Walter.

KWA MZIKI HUU BORA MSIJE, ONANA, MAXI GUMZO, YULE KIPA APEWA MIAKA MIWILI AFADHALI YA ROBERTINHO, SIO HUKO KWA GAMONDI NA HILI LA DABO SASA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply