Habari za Simba
Habari za michezo

HAO SIMBA HUKO SUPER LEAGUE, HAPA AL AHLY PALE MAMELODI SIO POA

Staff Desk August 28, 2023 5:46 pm

Droo ya African Football League (Super League) inatarajiwa kufanyika Septemba 2 huko Misri.

Simba Sc ni miongoni mwa timu nane ambazo zitashiriki michuano hiyo maalum ambayo inafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika.

Timu zimewekwa katika makundi mawili ya timu nne kulingana na alama walizokusanya katika mashindano ya CAF miaka mitano iliyopita.

Kundi A lina timu za Al Ahly, Mamelodi Sundowns, Wydad Athletic na Esperace. Kundi B lina timu za Simba, TP Mazembe, Enyimba na Perto Luanda.

Timu za kundi moja hazitakutana kwenye hatua ya awali kwa maana timu kutoka kundi A itapangwa kuchuana na timu kutoka kundi B.

Simba itafungua michuano hiyo Oktoba 20 kwa kuchuana na Al Ahly, Mamelodi Sundowns, Wydad au Esperance.

JEMEDARI AWASAGIA KUNGUNI YANGA KISA FEI TOTO GAMONDI AMCHAMBUA PACOME….MASTAA SIMBA WAONYWA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply