Habari za Azam FC
Habari za michezo

JEMEDARI AWASAGIA KUNGUNI YANGA KISA FEI TOTO

Staff Desk August 28, 2023 5:41 pm

Mchambuzi wa masuala ya soka nchini, Jemedari Said Bin Kazumari ameonyesha kuwashangaa mashabiki wa Klabu ya Yanga kufuatia vitendo vyao vya kumzodoa aliyekuwa mchezaji wao, Feisal Salum Abdallah ‘Fei Toto’.

Hii inakuja baada Fei Toto kuwanyoshea kidole mashabiki wa Yanga baada ya kufunga penati kwenye mchezo wao wa CAF dhidi ya Bahiri Kanema lakini mwisho wa siku Azam ilipoteza mchezo huo na kufungashiwa virago rasmi kwenye mashindano ya CAFCC.

Baada ya tukio hilo, mashabiki wa yanga walianza kumzodoa Fei mitandaoni wakisema kuwa ana kiburi ndiyo maana timu yake imeshindwa kufika mbali kwenye mashindano ya kimataifa.

“Kitu kimoja ambacho sijaridhika na watu Yanga, kwenye maisha tunasema ukishikwa shikamana, ukiachwa achika. Mashabiki wa Yanga wakubali kwamba Fei Toto sio mchezaji wao, hii habari ya kuanza kumsema kila anachofanya wanakosea.

“Fei ni kijana wetu, ameangalia maisha yake akaona atayapata Azam. Timu yake imeshacheza imetolewa, ameshamaliza, … heti huyu mtoto ana mdomo sana, ana kiburi ana maneno sijui nini…

“Jamani mambo ya kusema yule mwanamke nilikuwa nampeleka vacation Dubai, yeye ameshakubali kwenda Kzimkazi na mumewe mpya, jamani achikeni,” amesema Jemedari Said.

HUYU AZIZI KI MNAEMUONA NI ASILIMIA 40 TU HAO SIMBA HUKO SUPER LEAGUE, HAPA AL AHLY PALE MAMELODI SIO POA

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply